Psalms 74:3-8

3 aGeuza hatua zako kuelekea magofu haya ya kudumu,
uharibifu wote huu ambao adui ameuleta pale patakatifu.

4 bAdui zako wamenguruma pale ulipokutana nasi,
wanaweka bendera zao kama alama.
5 cWalifanya kama watu wanaotumia mashoka
kukata kichaka cha miti.
6 dWalivunjavunja milango yote iliyonakshiwa
kwa mashoka na vishoka vyao.
7 eWaliteketeza kabisa mahali pako patakatifu,
wakayanajisi makao ya Jina lako.
8 fWalisema mioyoni mwao,
“Tutawaponda kabisa!”
Walichoma kila mahali ambapo Mungu
aliabudiwa katika nchi.
Copyright information for SwhNEN